Friday, 26 May 2017

TIRA UMEZINDUA MFUMO WA UHAKIKI WA STIKA ZA BIMA BANDIA MKOANI MWANZA



Taasisi zinazojihusisha na utoaji wa huduma za bima zimetakiwa kutumia mfumo wa wa kielekitroniki wa TIRA MIS ili kuhepuka usambazaji wa stika bandia

Kauli hiyo imetolewa na kaim mkuu wa mkoa wa mwanza dk leonald Masale wakati wa uzinduzi wa mfumo wa kuhakiki stika kwa njia ya kielekitriniki

Masale amesema kufanya hivyo kutalisaidia taifa kupata mapato lakini pia jamii husika itanufaika na kuepuka kupewa stika za kughushi

Kwa upande wake kamishna wa bima nchini dk Baghayo saqware amesema kwamuda mrefu wateja wamekuwa wakiibiwa kwa kupewa stika za bima zisizostahili.

Aidha taifa limekuwa kipoteza mapato kutokana na kadhia hiyo na hivyo kwa kutumia mfumo huo mteja ataweza kuhakiki stika ya kile alichokilipia.

Subscribe to get more videos :