Friday, 26 May 2017

JAMII INATAKIWA KUWA MAKINI NA UGONJWA WA HOMA YA INI



Jamii imetakiwa kuwa  makini na ugonjwa wa homa ya ini ugonjwa ambao umekuwa ukileta madhara katika jamii .

Hayo yamesemwa na Dr. Edwin Masue ambaye ni daktari bingwa wa magonjwa ya ini alipokuwa akizungumza na city fm juu ya athari ambazo zinatokana na ugonjwa wa homa ya ini ugonjwa ambao kila kukicha unazidi kuwa ugonjwa hatari katika ukanda wa jangwa la sahara.

Dkt masue amesema kuwa ugonjwa huo unasababishwa na vitu mbalimbali kama ulaji wa vitu vyenye sumu lakini pia unaweza kuwapata watumiaji wa muda mrefu wa pombe kali .

Aidha ameitaka jamii kuwa  makini na kujiepusha na vitu ambavyo vinaweza kupelekea  kupata ugonjwa wa homa ya ini kwani wengi wao wanapoteza maisha kutokana na ugonjwa huo watu ambao ni nguvu kazi ya taifa

Subscribe to get more videos :