Friday, 26 May 2017

SERIKALI INAENDELEA KUCHUKUA HATUA MBALIMBALI KATIKA KUNUSURU MAISHA NA MALI ZA WANANCHI KUTOKANA NA KUWEPO KWA ONGEZEKO LA WANYAMA WAKALI NA WAHARIBIFU HAPA NCHINI.

Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kunusuru maisha na mali za wananchi kutokana na kuwepo kwa ongezeko la wanyama wakali na waharibifu hapa nchini.

Hayo yamesemwa leo bungeni jijini Dodoma wakati wa maswali na majibu na Mh.Waziri wa maliasili na utalii Profesa Jumanne Maghembe alipokuwa akijibu swali la Mh.Godluck Mringa mbunge wa jimbo la Uranga.

Profesa Maghembe ameongezea kwa kusema kuwa hatua hizo ni pamoja na kufanya doria za wanyama wakali na waharibifu ili kudhibiti madhara ya wanyamapori hao kwa kutumia Askari wa wanyamapori waliopo katika pori la seluhu eneo la Ironga,kikosi dhidi ya ujangiri pamoja na kutoa elimu juu ya uhifadhi  kwa jamii kuhusu kujikinga na wanyama hao wakali wakiwemo tembo na viboko.

Aidha amesema kuwa wizara imekuwa inafanya majaribio ya kutumia ngede zisizokuwa na Rubani kwa ajili ya kufukuza tembo pindi wanapovamia makazi na mashamba ya wananchi.

Subscribe to get more videos :