Saturday, 15 July 2017

RWANDA YAACHA KILIO KWA TAIFA STARS


July 15, 2017, timu ya Taifa ya Tanzania Taifa stars ilicheza mechi yake ya kwanza katika uwanja wa CCM KIRUMBA  kwa wachezazaji wanaocheza ligi za ndani ili kuwania tiketi ya ushiriki wa michuano ya  mataifa ya Afrika CHAN 2018, ambapo ililazimishwa sale ya gori 1-1 dhidi ya timu ya taifa ya RWANDA.



Mchezaji  Dominique Nshuti wa timu ya taifa ya Rwanda aliiandikia bao la kuongoza timu yake dakika ya 17 kufuatia makosa yaliyofanywa na mchezaji wa Taifa Stars ambae ni majeruhi Shomari kapombe ambae alitoka na kuingia Boniface maganga


Mchezo wa vuta nikuvute huku timu zote mbili zikionyesha uwino sawa uwanjani, Taifa stars walifanikiwa kusawazisha goli na kubadili matokeo dakika ya 34 kupitia nahodha wake Hamid Mao  kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji Mico Juastin kuunawa mpira katika eneo la hatari na kufanya matokeo kuwa Taifa stars 1-Rwanda 1.

Timu zote mbili zilifanya mabadiliko ambapo Taifa stars walimtoa mchezaji John Bocco na nafasi yake kuchukuliwa na Stamil Mbonde na kufanya mchezo kubadilika japo mabadiliko hayo hayakuzaa matunda.

Hadi mchezo unamalizika mabao yalikuwa 1-1 ambapo sasa Taifa Stars wanakibarua kikubwa katika mchezo wa marudiano, mchezo utakaochezwa Kigali- Rwanda tarehe 23 mwezi wa saba 2017 na ili Taifa stars ifuzu kuingia hatua inayofuata inatakiwa ishinde kuanzia 1-0 au kama ni sale basi iwe sale kuanzia mabao 2-2.

 





Subscribe to get more videos :