Monday, 29 May 2017

ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA UKATILI WA MTOTO WAKE

KAMANDA WA POLIS MKOA WA MWANZA
AHMED MSANGI 



Mtu mmoja anashikiliwa na jeshi la polis mkoani mwanza  kwa kumfanyia ukatil mwanae  .
Tukio hilo limetokea may  25.05.2017 majira ya saa 05:00hrs alfajiri katika mtaa wa Ndofe wilaya ya Nyamagana Jijini Mwanza, Bw Nuhu James miaka 50 mkazi wa Ndofe, anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumfanyia ukatili mtoto wake aitwaye wa kiume miaka 14, mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya secondary Igoma kwa kumfunga kamba miguuni na mikononi kisha kumchapa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na baadae kumkata na kisu sehemu za makalio, kitendo ambacho ni kinyume na sheria.
Inasemekana kuwa baada ya mama wa mtoto kuona ukatili aliofanyiwa mtoto wake na hali yake ya kiafya kuzidi kubadilika alishindwa kuvumilia ndipo  tarehe 28.05.2017 alikwenda kituo cha polisi kutoa taarifa. Askari walifanya ufuatiliaji wa haraka kuhusiana na taarifa hizo na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa aliaamua kumfanyia ukatili wa aina hiyo  mtoto wake baada ya kugundua kwamba mwanae ni mtoro shuleni. Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa, pindi uchunguzi ukikamalika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani, majeruhi amepelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu na hali yake inaendelea vizuri.
Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa wakazi wa jiji na mkoa wa Mwanza hususani wazazi/walezi kuacha tabia ya kuwapa adhabu ya vipigo watoto pindi wanapokosea bali wanatakiwa wakae na watoto wao kisha wawaelimishe kuhusu maadili mema na mabaya, ili kuepusha matatizo ya aina kama hii kwa wazazi, au ajali na vifo vinavyoweza kuzuilika. 

Subscribe to get more videos :