Saturday, 27 May 2017

AMUUA MKE KWA RISASI KISHA KUJIUA MWENYEWE


Katika hali isiyokuwa ya kawaida mfanyabiashara wa samaki jijini Mwanza Bw. Maxmiliani Ngedele  mwenye umri wa miaka 40 mkazi wa mtaa wa Kanyerere Kata ya Butimba wilayani Nyamagana mkoani Mwanza amemuua mkewe kwa kumpiga risasi Mgongoni na kutokea tumboni  kisha yeye kujiua kwa kujipiga risasi kifuani
.
Tukio hilo limetokea usiku wa Tarehe 25 mwezi huu majira ya saa tano usiku  katika nyumba yao iliyopo mtaa huo baada ya kutokea sintofahamu kati ya wanandoa hao hali iliyopelekea mume kuchukua maamuzi magumu ya kumpiga risasi mkewe aitwae Tedy Patrick miaka 38  na yeye kujiua kwa kujipiga risasi.

Mtoto wa marehemu hao aitwaye Ester Maximillian alieleza kuwa, Siku ya tukio baba yake Bw. Maximilian alifika nyumbani majira ya saa nne usiku akitokea kazini kwake na yeye ndio alimfungulia mlango na wakasalimiana vizuri lakini wakati mama yake Bi. Tedy Patrick akifika nyumbani kwake majira ya saa tano usiku na alifunguliwa mlango na mfanyakazi wao,

Baada ya mfanyakazi kumfungulia mama mlango alikuja na kunieleza kuwa mama amelewa kweli alipoingia ndani alikuja hadi chumbani kwetu akiwa naongea maneno ambayo siyo mazuri huku baba akiwa amekaa kimya na baada ya hapo waliingia chumbani kwao na kujifungia na sisi tukaingia chumbani kwetu,
Lakini baada ya muda tukasikia milio ya risasi na kelele za baba akisena nataka kujiua tulipoenda nikamwambia baba usijiue kwani utatuacha na nani hapo nikasikia mama anamuomba msamaha baba kuwa amsamehe kwa kile kilichotokea baada ya hapo sisi tukarudi chumbani,
Lakini baada ya muda tulisikia mlio wa risasi tulipoenda tukakuta mama anavuja damu huku baba akiwa amekufa tayari na neon la mwisho alilotuambia mama alisema mnikimbize hospital kwani amebaki yeye tu wa kuwasaidia,
Na tulivyoita majirani wakamkimbiza hospital kwa ajili ya matibabu lakini na yeye amefariki akiwa hospital akipatiwa matibabu.
Ester aliendelea kueleza kuwa hajawahi kuona wazazi wake wakigombana hadi kupigana bali walikuwa wanakaa pamoja wakati wa jioni na kushauriana mambo mbalimbali ya kimaisha na biashara zao lakini ugomvi haukuwepo.
Jirani wa marehemu yao aliyejitambulisha kwa jina la Jani Malegesi alisema siku ya tukio walisikia milio ya risasi wakadhani mtaa umevamiwa na majambazi wakati wanatafakari nini kinatokea katika mtaa wao wakasikia mlinzi wa jirani yao huyo akiwaita kuwa wanahitaji wakatoe msaada na walipofika walikuta damu nyingi zimezagaa katika chumba cha wanadoa hao huku Maximillian akiwa amekata roho,
Ikanibidi niwatulize wale watoto na baada ya hapo nilipiga simu polisi na walipo kuja tulimpeleka Tedy Hospital kwa ajili ya matibabu lakini alfajiri ya kuamkia Tarehe 26 tukapata taarifa kuwa naye amefariki dunia,
Kweli hatukuwahi kusikia kama wanaugomvi wa aina yeyote kwani wanamuda mchache sana tangu walipohamia kwenye nyumba yao hiyo.
Mwenyekiti wa mtaa wa Kanyerere Bw. William Ngongo alieleza kuwa taarifa alizipata majira ya saa 11 alfajiri jambo ambalo lilimfanya kufika kwenye tukio na alipofika alikuta mwili wa marehemu umepelekwa hospital na mama wa familia na naye alikuwa amekufa kwa kweli tumesikitishwa sana kutokana na familia hii nilikuwa naifahamu vizuri sana,

Bw. William alisema jeshi la polisi linatakiwa na serikali wanatakiwa kutoa silaha kwa kuangalia mtu ambaye wanampa silaha za moto ili kupunguza matukio kama hayo yanayojitokeza katika maeneo mbalimbali hapa nchini hasa kwa kuwahusisha viongozi wa serikali za mitaa ili waweze kuja watu wanaomiliki silaha katika mitaa yao.

Kamanda wa polis mkoani Mwanza Naibu kamishina wa polisi Ahmed Msangi amesema kuwa taarifa za awali zinabainisha kuwa wawali hao  walitokea  kutoelewana  ndani ya nyumba hiyo ndipo majirani waliposikia milioni ya riasi kisha kufika na kukuta mwanaume akiwa amelala tayari amepoteza  maisha huku mwanamke akiomba msada na kukimbizwa hospital ambapo amefariki wakati akipewa matibabu
kamanda Msangi amesema kuwa chanzo cha tukio hilo la wanandoa hao bado halijafahamika kutokana na wote  kupoteza maisha lakini uchunguzi bado unaendelea ili kubaini chanzo cha tukio hilo.
Hata hivyo Kamanda Msangi amewataka wakazi wa jiji la Mwanza iwapo wanamatatizo ya kifamilia hususani masuala ya mali,mahsusiano ni vyema kufika kwa viongozi wao wa mtaa pamoja na viongozi wao wa dini ili kupata ushauri na kuepusha madhara makubwa yanayoweza kutokea ikiwamo vifo na kuacha watoto katika mazingira magumu ya maisha.

Aidha alisema kutokana na matukio kama hayo kujitokeza mara kwa mata jeshi la polisi mkoa wa mwanza linajipanga kutengeneza mfumo mzuri wa kuwamilikisha watu silaha ikiwemo mtu kupimwa akili ili kupunguza matukio ya aina hiyo.

Subscribe to get more videos :